ON POINT MEDIA

ON POINT MEDIA
Karibuni sana kwa kazi nzuri ya video za harusi mikutano na kadharika

SHIRKA LA NYUMBA LA TAIFA

SHIRKA LA NYUMBA LA TAIFA
NYUMBA YANGU MAISHA YANGU

Thursday, 22 December 2016

WAZIRI LUKUVI ATEMBELEA MIRADI YA NHC MUSOMA


 Jengo la Biashara la Musoma Mjini lililojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambalo Waziri Lukuvi alifika kuangalia maendeleo yake.


 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwa ndani ya jengo hilo.


 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwa ndani ya jengo hilo.

 Waziri Lukuvi akikagua nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) eneo la Buhare wilayani Musoma lenye jumla ya nyumba 50 zinazokaribia kukamilika.



Friday, 21 October 2016

SHULE YA SEKONDARI KUSUNGU YA ILALA YAPOKEA VITI KUTOKA TPDC

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limekabidhi viti 142 vyenye thamani ya shilingi milioni 6 katika Shule ya Sekondari Kisungu iliyopo kata ya Kinyerezi jijini Dar es Salaam. 

Meneja Mawasiliano wa TPDC, Marie Msellemu akikabidhi viti hivyo kwa niaba ya Mkurungezi Mtendaji wa TPDC amesema viti hivyo vitasadia kutatua changamoto ya wanafunzi kukosa viti shuleni hapo. 

Amengoze kuwa mchango huo wa viti ni kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika kuhakikisha wanafunzi wanakuwa na mazingira rafiki ya kujifunzia. 

Shirika hilo limekuwa na utaratibu wa kuchangia jamii katika nyaja za afya, elimu, maji, utawala bora na michezo kupitia programu yake kuwajibika kwa jamii.
Mkuu wa shule ya Sekondari Kisungu, Mkama Mgeta (kulia) na wanafunzi wa Shule ya Sekondari wakipokea kiti kutoka kwa Meneja Mawasiliano wa TPDC, Marie Msellemu (kushoto) katika hafla fupi ya kupokea viti 142 kutoka TPDC.
 Meneja Mawasiliano wa TPDC, Marie Msellemu akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC katika hafla fupi ya kukabidhi viti 142 vyenye thamani ya shilingi milioni 6 katika kwa Shule ya Sekondari Kisungu iliyopo kata ya Kinyerezi jiji Dar es Salaam.
 
Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Kisungu, Philimina Casimr akisoma taarifa ya Shule hiyo kabla ya kupokea viti kutoka TPDC.
 Sehemu ya viti 142 vilivyotolewa na TPDC.

PROFESA Sospeter Muhongo Afunguka Kuhusu Madini Kuchangia Pato la Taifa Kwa Asilimia 10

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amesema hadi kufikia mwaka 2025, sekta ya madini nchini inapaswa ichangie asilimia 10 kwenye Pato la Taifa.

Katika kipindi cha mwaka 2015 sekta hiyo imechangia asilimia 4.3 kutoka asilimia 3.7 kwa mwaka 2014, kiasi ambacho waziri huyo amesema bado ni kidogo.

Aliyasema hayo mjini Dodoma jana mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini wakati akitoa taarifa kuhusu shughuli za utafutaji madini na maendeleo ya sekta ya madini.

Hata hivyo, alitaja changamoto zinazoifanya sekta hiyo kuwa na mchango mdogo katika Pato la Taifa kuwa ni pamoja na kushuka kwa bei ya madini kwenye soko la dunia na kutokuanzishwa kwa migodi mingine mikubwa ya uchimbaji hivi karibuni.

Alisema kwa sasa uwezo wa uzalishaji wa dhahabu kwa migodi yote nchini ni wakia milioni 1.25 kwa mwaka na uzalishaji kuanzia mwaka 2011 hadi 2015 ni wakia milioni 5.68 sawa na tani 176.7 yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 9.06 sawa na Sh trilioni 19.7.

Waziri huyo alifafanua kuwa ipo mipango mbalimbali ya kuendeleza shughuli za madini nchini ikiwemo kuboresha ukusanyaji na usambazaji wa taarifa na takwimu za kijiosayansi, udhibiti wa utoroshwaji wa madini na ukaguzi katika shughuli za uzalishaji madini.

Naye Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche alitaka kujua hatua zinazochukuliwa dhidi ya tuhuma za utoroshaji wa madini unaofanyika katika baadhi ya migodi ikiwemo mgodi wa Accacia ambao ndani ya mgodi kuna kiwanja cha ndege. 

Serikali Yapunguza Deni La Mifuko Ya Hifadhi Ya Jamii


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali tayari imeshalipa sh. bilioni 722.7 kati ya sh. bilioni 964.2 za madeni ya michango ya jumla ambayo Serikali inadaiwa na mifuko ya hifadhi ya jamii nchini.

Ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Oktoba 20, 2016) wakati akifungua Mkutano wa Sita wa wadau wa NSSF ulioanza leo kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Arusha na kuhudhuriwa na washiriki zaidi ya 600.

Amesema sekta hiyo imekua kwa asilimia 15 kutoka sh. trilioni 8.9 mwaka 2015 hadi kufikia sh. trilioni 10.2 mwaka 2016. “Hadi kufikia Juni 2016, takwimu zinaonesha idadi ya wanachama imeongezeka na kufikia milioni 2.1. Rasilmali za mifuko zimefikia shilingi trilioni 10.28 na mafao yaliyolipwa kwa kipindi cha mwaka kinachoishia Juni 2016 ni shillingi trilioni 2.93. Michango ya wanachama kwa mwaka ni shilingi trilioni 2.15 uwekezaji katika nyanja mbalimbali umefikia kiasi cha shilingi trilioni 9.29,” ameongeza.

Waziri Mkuu pia amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara awaandikie barua waajiri wote wanaodaiwa na shirika hilo na kuwataka wawasilishe fedha wanayodaiwa mara moja na wale ambao hawatalipa ndani muda utakaowekwa wafikishwe mahakamani na yeye apewe taarifa.

“Kumekuwepo na changamoto ya muda mrefu ya baadhi ya waajiri kutolipa michango kwa wakati hali inayoleta usumbufu mkubwa kwa wanachama hasa wanapofikia muda wa kustaafu. Suala hili halikubaliki, hivyo natoa maelekezo kwa waajiri wote nchini waheshimu sheria na wawasilishe michango yao kwa wakati,” amesisitiza.

Mbali ya kuwabana waajiri, Waziri Mkuu pia amewataka wanunuzi wa nyumba za shirika hilo na wapangaji wote wanaodaiwa wakamilishe malipo yao na wasipofanya hivyo ndani ya muda uliopangwa wafikishwe mahakamani.

“Nimeambiwa pia lipo tatizo la wadaiwa wa nyumba yaani wanunuzi na wapangaji. Suala hili lilitolewa maelekezo na Waziri wa Nchi, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu. Nataka nisisitize kuwa watu wote walionunua nyumba za NSSF na bado hawajakamilisha malipo na wale waliopanga lakini hawalipi kodi wanatakiwa kulipa haraka au wakabidhi nyumba hizo kwa NSSF ziuzwe kwa watu wengine, vinginevyo nao wafikishwe mahakamani.”

Akizungumzia utendaji wa shirika hilo, Waziri Mkuu amewapongeza viongozi wa shirika hilo na Bodi ya Wadhamini kwa uamuzi wake wa kuwekeza kwenye uzalishaji wa sukari nchini. Amesema kiwanda kitakachojengwa, kinatarajiwa kutoa ajira zaidi ya 100,000 kwa Watanzania na hivyo kuongeza wanachama katika mfuko wa NSSF.

“Nimefurahishwa na uamuzi wa NSSF na PPF kuungana ili kukabiliana na tatizo la sukari nchini. Tumeelezwa hapa kuwa mashirika haya yatashirikiana kujenga Kiwanda cha Sukari kitakachozalisha tani 200,000 kwa mwaka. Kiwanda hicho kitajengwa katika eneo la Mkulazi lililopo mkoani Morogoro,” amesema.

Mapema, akielezea utendaji wa shirika hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof. Godius Kahyarara alisema limeboresha mafao ya wanachama wake kutoka sh. 80,000 hadi sh. 100,000 kwa mwezi.

Alisema limeanza kufanya upembuzi yakinifu wa kujenga nyumba za watumishi Dodoma ili kuendana na uamuzi wa serikali kuhamia Dodoma. “Upembuzi bado unaendelea lakini tumeshabaini kuna uwezekano wa kujenga nyumba 200 hadi 300 mkoani Dodoma,” alisema.

Kuhusu uwekezaji kwenye ujenzi wa Daraja la Mwalimu Nyerere lililopo Kigamboni, Dar es Salaam, Prof. Kahyarara alisema uwekezaji huo unalipa kwa sababu makusanyo ya tozo kwa watumiaji yamefikia asilimia 109. “Tuna uhakika kwamba fedha tulizowekeza zitarudi,” amesisitiza.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amepokea msaada wa tani 45 za saruji ambazo ni sawa na mifuko 900 yenye thamani ya sh. milioni 15 kwa ajili ya waathirika wa tetememo la ardhi mkoani Kagera. Amepokea msaada huo kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya NSSF, Prof. Samuel Wangwe.

Akiwasilisha msaada huo, Prof. Wangwe alisema wameguswa na tatizo lilitokea mkoani Kagera na wameamua kutoa mchango ili kusaidia juhudi za Serikali kukabiliana na maafa hayo. Pia alisema wamekamilisha ahadi yao ya madawati 6,000 yenye thamani ya sh. milioni 400 ambayo waliitoa awali.

Waziri Mkuu aliwashukuru kwa misaada hiyo na kuwahakikishia kwamba itafikishwa kwa walengwa.

Kikosi Kazi Cha Jeshi La Wananchi (JWTZ) Cha Wasili Kagera Kwa Ajili Ya Kujenga Miundombinu Iliyoathiriwa Na Tetemeko La Ardhi


Kikosi kazi cha jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ)kutoka makao makuu ya Jeshi kimewasili Mkoani Kagera kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya serekali iliyoathiriwa vibaya na tetemeko la ardhi lililotokea Mkoana Kagera septemba 10 mwaka huu.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa kituo cha afya katika kijiji cha Kabambyaile Kata ya Ishozi Wilaya ya Missenyi, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu alisema kuwa kikosi hicho kinawataalamu wa fani zote za ujenzi na wamekuja na vifaa vyote vya ujenzi.

"Hiki kikosi kitafanya kazi kwa masaa 24 yaani watajenga usiku na mchana taasisi zote za umma zilizoathiriwa na tetemeko ikiwa ni pamoja na mashule na zahanati ili watoto waende shule na wagonjwa waendelee kupata matibabu"alisema.

Alisema mpaka kufikia july mwakani ujenzi wa miundombinu utakuwa umekamilika kwa robo tatu na aliwataka wananchi wawape ushirikiano maeneo yote watakayopita kujenga miundombinu ya umma.

Kiongozi wa kikosi hicho Meja Buchadi Kakura alisema kuwa kikosi hicho kimekuja Kagera kusaidia serekali ya Mkoa kurudisha miundombinu yote ya umma iliyoathiriwa na tetemeko la ardhi katika hali yake ya kawaida.

"Ni vigumu kusema lini tutakamilisha ujenzi ila sisi tutafanya kazi usiku na mchana ili ujenzi huu ukamilike ndani ya muda mfupi"Alisema Meja Kakura.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salimu Kijuu(mwenye Suti)akisikiliza maelezo juu ya kikosi kazi cha askari waliokuja kujenga miundo mbinu ya umma iliyoathiriwa na tetemeko la ardhi

Friday, 23 September 2016

Kikwete Atunukiwa Tuzo Ya Uongozi Wa Kisiasa Na Utetezi Seebait.com 2016



 Na  Mwandishi Maalum, New York

Shirika lisilo la  Kiserikali    la Speak  Up for Afrika    limemtunukia tuzo, Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete kutokana na uongozi wake wa kisiasa na utetezi wake  kwa  makundi ya jamii yaliyo katika mazingira magumu hususani wanawake na watoto.
  
Utoaji wa  Tuzo hiyo  ya  uongozi wa kisiasa na utetezi , umekwenda sambamba na   hafla ya  miaka mitano ya kuanzishwa kwa  Taasisi ya Speak up  Afrika. Hafla  hiyo iliyofanyika jana Alhamisi Jijini New York   ilikuwa  pia  ni sehemu ya kuhamasisha uchangiaji   wa shughuli za  Taasisi hiyo.
  
Mchango ambao umetambuliwa na  Speak Up  Afrika,   taasisi ambayo imekuwa ikifanya kazi  kwa Karibu na Rais Mstaafu Kikwete, ni  katika maeneo ya  upelekaji na usambazaji wa huduma za msingi za afya hususani afya ya mama na mtoto,  udhibiti wa  ugonjwa  wa malaria kupitia kampeni  ya malaria haikubaliki ,usambazaji wa vyandarua  vyenye viatilifu, kampeni ya  lishe bora, na  kampeni ya   chanjo kwa watoto.
  
Pamoja  na  kutambua  juhudi za   Rais Mstaafu  Kikwete katika  kuyasemea maeneo hayo,  Taasisi hiyo kupitia  Mkurugenzi wake  Mtendaji Bi. Kate Campana pia imemtambua  kama kiongozi ambaye    amekuwa mstari wa mbele  wa kulisema Bara la Afrika kila  mara alipopata  fursa  ya  kufanya hivyo wakati akiwa madarakani na hata baada ya kustaafu.
  
Rais kikwete ameelezwa katika hafla hiyo iliyowashirikisha  wadau wa kada mbalimbali, kama kiongozi wa kisiasa ambaye amezigusa nyoyo za watu wengi kujitolea kwaajili ya watu wenye mahitajio ya kupata huduma za msingi za kijamii ambazo  au wameshindwa kuzipata kutokana na kipato kidogo au haziwafikii kabisa.
  
Akipokea  Tuzo hiyo, Rais  Mstaafu Kikwete , amesema Tuzo hiyo ni ya watoto wote  waafrika ambao ndio  waliomfanya asimame   mbele ya wageni waalikwa.
  
“ Ni kwa sababu yenu ndio sababu nimetenga muda wangu  baada ya kustaafu kusukuma mbele agenda ya  kuboresha maisha yanu. Ninafanya hivyo kwasababu makuzi yangu yalikuwa kama  ya mtoto yeyote yule wa  kiafrika, nimeyaishi maisha  wanayo ishi. Na kwa hiyo ninaelewa fika  hamu na kiu yao ya kuwa  na maisha bora na afya njema”. Akasema Kikwete na kushangiliwa na wageni waalikwa.
  
Akaongeza kuwa  ,  mafaniko ambayo ameyapata katika  juhudi hizo  za kufikisha huduma za msingi  za kijamii kwa makundi  yenye mahitaji  yametokana na mambo mawili makubwa moja ni   aina ya uongozi  alioutumia kusukuma harakati hizo. Na pili  uhamasishaji uliofanyika katika  kupiga vita malaria kupitia Speak Up Afrika na    kampeni yao ya  malaria haikubaliki.
  
“ Nisingeweza kuyafanya niliyoyafanya   bila uungugwaji mkono na  ushirikiano  wa karibu nilioupata  na ninaoupata kutoka taasisi za kimataifa  ikiwamo hii ya  Speak Up  Afrika. Ndio maana  kwa mfano,  tumeweza kupunguza visa vya malaria kwa   theluthi mbilli,  tumefanikisha  upatikanaji wa chanjo kwa asilimia 96 kwa watoto wote na kupunguza vifo vitokanavyo na  malaria kwa   nusu.” Akaeleza Kikwete na kushangiliwa  tena.
  
Akasema, anamini katika ushirikiano na wadau mbalimbali  kama akina Ray Chambers kupitia kampeni ya  hakuna tena malaria, Taasisi ya  Bili na Melinda Gates na Gavi Vaccination   Alliance ambayo anashirikiano  nayo kwa karibu katika  kampeni ya chanjo kwa wote.
  
Rais  Mstaafu amewahakikishia   watendaji wa Speak  Up Afrika kwamba  ataendelea kufanya kazi nao kwa karibu  kutokana  kile alichosema amejionea mwenye kazi nzuri wanayoifana.
  
 Akawasihi  wadau mbalimbali  kuichangia taasisi hiyo  kwa kile alichosema, inafanya kazi kubwa  ya siyo tu kufikisha huduma za kijamii pale zinapotakiwa lakini  pia imekuwa ni kipaza sauti cha Afrika.
  
Wengine waliopewa Tuzo kwa kutambua michango yao kwa jamii ni  pamoja na   Professa Awa Marie Coll- Seck, Waziri wa Afya  wa Senegal, Bibi Toyin  Saraki,  mwanzilishi wa Taasisi ya  Wellbeing  Afrika ambayo  pia imekuwa ikitoa  elimu na misaada kwa wanawake na watoto pamoja na elimu  kwa wakunga na kutambua kazi nzuri, kubwa na ngumu  ya kuwahudumia wanawake wenzao wanapojifungua.  Na  Bwana Kabirou Mbodje ambaye ni Mkurugenzi mtendaji wa  Taasisi ya  Wari.
  
Taasisi ya  Speak  Up  Afrika  imeanzishwa  na wanawake na inaongozwa na wanawake. Ni taasisi ambayo imejijengea uweo na sifa kubwa ndani  ya kipindi cha miaka mitano tangu  kuanzishwa kwake

Thursday, 15 September 2016

Mabaki yaliyopatikana Pemba, Tanzania ni ya MH370


Mabaki ya ndege yaliyopatikana Pemba
Image copyrightSERIKALI, TANZANIA
Mabaki ya ndege yaliyopatikana katika pwani ya visiwa vya Pemba nchini Tanzania yalitoka kwa ndege ya shirika la Malysia Airlines iliyotoweka mwaka 2014, maafisa wa Malaysia wamethibitisha.
Waziri wa uchukuzi wa Malaysia Liow Tiong Lai amesema kupitia taarifa, kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, kwamba baada ya uchunguzi imebainika kwamba kipande hicho kikubwa cha bati kilichopatikana mwezi Juni ni cha ndege hiyo safari nambari MH370.
Amesema uamuzi huo ulifikiwa na wataalamu kutoka Idara ya Usalama wa Safari za Ndege ya Australia (ATSB) na wale wa kuchunguza usalama wa MH370.
Mapema Julai, waziri wa uchukuzi wa Australia Darren Chester alikuwa amedokeza kwamba kulikuwa na uwezekano mkubwa mabaki hayo yalikuwa ya ndege hiyo.
Alisema muundo wa mabaki hayo, ukubwa wake na muonekano wake viliashiria kwamba yalikuwa ya ndege hiyo ya Malaysia.
Mabaki hayo pia yalikuwa na muhuri wa kuonesha tarehe ya kuundwa kwake ambayo ilikuwa Januari 23, 2002. Ndege hiyo ya Malaysia iliwasilishwa kwa shirika hilo 31 Mei, 2002, kwa mujibu wa tovuti ya shirika la Channel News Asia.
Ndege hiyo aina ya Boeing 777 ilitoweka Machi 2014, ikiwa na abiria 239 baada ya kupaa kutoka Kuala Lumpur, mji mkuu wa Malaysia kuelekea Beijing.
Bw Liow amesema mabaki hayo yatachunguzwa zaidi kubaini iwapo kutapatikana ufumbuzi kuhusu kilichotokea hadi ndege hiyo ikatoweka.
Awali, wachunguzi walikuwa wamethibitisha kwamba mabaki yaliyopatikana visiwa vya Reunion mwezi Julai 2015 yalitoka kwa ndege hiyo.
Mabaki mengine yanayodhaniwa kutoka kwa ndege hiyo yamepatikana Msumbiji, Afrika Kusini na visiwa vya Rodrigues, Mauritius.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya Septemba 14

PICHA: MAKAMU WA RAIS ALIPOMWAKILISHA RAIS MAGUFULI KWENYE SHEREHE ZA KUAPISHWA KWA RAIS WA AWAMU YA 6 WA ZAMBIA

lungu

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu  Septemba 13, 2016.
 Rais Robert Mugabe akisalimiana na Rais wa Kwanza wa Zambia Dkt Kenneth Kaunda
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Botswana Luteni Jenerali Seretse Khama baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akiwa na Naibu Rais wa Kenya Mhe william Rutto,  Makamu wa Rais wa Namibia Mhe. Nickey Iyambo na Rais wa kwanza wa Zambia Dkt. Kenneth Kaunda baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu Septemba 13, 2016
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akiwa na Naibu Rais wa Kenya Mhe william Ruttona wageni wengine wakielekea jukwaani  kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka ambako amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu Septemba 13, 2016.
 Rais mteule wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu akila kiapo kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kwenye sherehe za kuapishwa kwake kuwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia  Septemba 13, 2016
Rais Robert Mugabe wa Zambia akizungumza kwa niaba ya viongozi waalikwa wote
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akimpongeza Makamu wa Rais  wa Zambia Mama Inonge Mutukwa Wina kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu Septemba 13, 2016
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akinong’onezwa jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Vijana, Michezo na Maendeleo ya watoto Mhe. Agnes Musunga baada ya sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu  Septemba 13, 2016