ON POINT MEDIA

ON POINT MEDIA
Karibuni sana kwa kazi nzuri ya video za harusi mikutano na kadharika

SHIRKA LA NYUMBA LA TAIFA

SHIRKA LA NYUMBA LA TAIFA
NYUMBA YANGU MAISHA YANGU

Monday, 18 March 2019

HALMASHAURI ZATAKIWA KUINGIA MKATABA NA NHC KUJENGA NYUMBA

HALMASHAURI ZATAKIWA KUINGIA MKATABA NA NHC KUJENGA NYUMBA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa William Lukuvi amezitaka halmashauri nchini kuingia mkataba na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa ajili ya ujenzi wa Nyumba na Ofisi kutokana na  Shirika hilo kuwa na uzoefu wa kujenga nyumba zenye ubora na gharama nafuu.

Lukuvi aliyasema hayo tarehe 18 Machi 2019 wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi na Maliasili na Utalii ilipotembelea mradi wa ujenzi wa nyumba 20 katika eneo la chatur Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga. Kati ya nyumba hizo, kumi ni za Halmashauri ya Wilaya ya Muheza na nyumba nyingine kumi ni za Shirika la Nyumba.

Alisema, wakati wa kuingia mkataba  wa ujenzi wa Nyumba au Ofisi Halmashauri hizo zinapaswa  kuwa na fedha pamoja na kuandaa miundo mbinu (Maji, Umeme n.k) ili kuepuka kuchelewa kukamilisha ujenzi. 


Mh. Lukuvi amelipongeza Shirika kwa kuendelea na ujenzi wa nyumba hizo licha ya Halmashauri kuchelewesha malipo kwa ajili ya ujenzi huo..

Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakiongozwa na Kaimu Mwenyeketi wake Shaban Shekilindi walihoji kuchelewa kwa mradi wa ujenzi wa nyumba hizo za Halmashauri lakini walielezwa hali hiyo imesababishwa na Halmashauri kuchelewesha malipo ya  fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza Nassib Mmbaga aliwaambia wajumbe wa Kamati kuwa Halmashauri yake ilichelewa kutoa fedha za ujenzi kwa wakati kutokana na kutumia fedha kujenga madarasa kufuatia kuwepo idadi kubwa ya wanafunzi wa shule za msingi ambao wana uhaba wa madarasa. Hata hivyo, Mkurugenzi huyo Mtendaji alieleza kuwa tatizo hilo lishatatuliwa na kuahidi kulipa kiasi cha  fedha kilichobakia kulingana na mkataba.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alilitaka Shirika la Nyumba la Taifa kufanya kazi kibiashara na kuacha tabia ya kufanya kazi kwa ushawishi wa mtu au kisiasa kwasasbu kwa kufanya hivyo kutapelekea kutouzika kwanyumba zinazojengwa hivyo Shirika litaingia kwenye hasara.
 

Mradi wa nyumba 20 uliopo eneo la chatur katika Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.

  Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Lukuvi (Aliyesimama) akisoma taarifa ya Wizara kwa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

Baadhi ya wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa Dkt. Maulidi Banyani alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi wa nyumba za makazi chatur

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika, Dkt. Maulidi Banyani alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi wa nyumba 20 za makazi unaotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa 



 Kaimu Mwenyeketi wa  kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii  Shaban Shekilindi mwenye shati jeupe ( wa pili kutoka kulia)  akiongozana na Mwenyekiti wa Bodi ya shirika la nyumba la Taifa Dkt. Sophia Kongela (wa kwanza kutoka kulia), Mkurugenzi Mkuu Dkt. Maulidi Banyani (wa pili kutoka kushoto) pamoja na Mkuu wa kitengo cha ukaguzi wa ndani wa Shirika Bw. Abdallah Migila (wa kwanza kushoto).
  Mhe. Lukuvi Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi (wa pili kutoka kulia) pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Agelina Mabula ( mwenye reflector ya njano) wakiwa na wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii walipotembelea mradi wa makazi uliopo katika eneo la chatur 
 wilaya ya Muhuza



  Mhandisi Mannig Mwalwaka ambaye ndie msimamizi wa mradi huo akitoa maelezo ya mradi huo

Thursday, 24 January 2019

NAIBU WAZIRI DK MABULA ARIDHISHWA NA UJENZI WA NHC KATIKA MJI WA SERIKALI MTUMBA

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angeline Mabula ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa ofisi za wizara katika mji wa serikali ya Mtumba mkoani Dodoma unaojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
Dk Mabula alitoa kauli hiyo leo tarehe 22 Januari 2019 wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa ofisi za Serikali katika mji wa Mtumba mkoani Dodoma unaojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambalo liko chini ya Wizara yake.
Alisema kazi inayofanywa na shirika la Nyumba la Taifa kujenga ofisi za Serikali katika mji huo kwa sasa unaenda kwa kasi na unatia moyo jambo linalooonesha kuwa mradi wa ujenzi wa ofisi hizo utakamilika katika muda uliopangwa.
Katika mradi huo Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kupitia kampuni yake ya ujenzi inajenga ofisi za Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Fedha na Uchumi, Wizara ya Nishati pamoja na Wizara ya Viwanda na Biashara.
Aidha, Dk Mabula amefurahishwa na ufuatialiaji wa ujenzi wa ofisi hizo unaofanywa na Wizara ya Fedha pamoja na Viwanda na Biashara na kueleza kuwa hatua hiyo inalifanya Shirika hilo kufanya kazi kulingana na mahitaji ya wateja wake.
Alibainisha kuwa, pamoja na changamoto ya kukatika umeme lakini NHC imejitahidi na kilichomfurahisha ni kuwepo vifaa vyote vya ujenzi kwenye eneo la ujenzi jambo linalompa faraja kuwa hakuna kitakachokwamisha ujenzi kukamilika kwa wakati
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amepongeza jitihada znazofanywa na Rais John Pombe Magufuli za kuhamishia Makao Makuu ya Serikali Dodoma na kubainisha kuwa hatua hiyo inatimiza ndoto ya baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Naye Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Emma Lyimo alilisifu Shirika la Nyumba la Taifa kwa kasi kubwa wanayoendelea nayo kwenye ujenzi wa ofisi ya Wizara yake na kubainisha kuwa pamoja na kuchelewa kuanza ujenzi lakini kasi wanayoenda nayo ana imani ujenzi utakamilika kwa wakati.
Naye Msimamizi wa ujenzi wa ofisi ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo la Makazi Mhandisi Grace Musita alisema, ujenzi wa ofisi umefikia asilimia sabini na tano na anatarajia utakamilika katika tarehe iliyopangwa kwa kuwa wamefikia hatua nzuri ya kukamika.

 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akiangalia maendeleo ya Ujenzi ya Ofisi ya Wizara ya Nishati katika mji wa Serikali wa Mtumba, kushoto ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Elisante Ulomi na katikati ni Mkurugenzi wa uendelezaji miliki Shirika la Nyumba la Taifa Haikameni Mlekio.


  Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akioneshwa moja ya kifaa kitakachotumika katika Ujenzi ya Ofisi ya Wizara ya Nishati katika mji wa Serikali wa Mtumba mkoani Dodoma, kulia ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Elisante Ulomi na kushoto ni Mkurugenzi wa uendelezaji milikShirika la Nyumba la Taifa Haikameni Mlekio.


 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akimsikiliza Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Viwanda na Bisahara Emma Lyimo (Kulia) wakati alipotembelea maendeleo ya Ujenzi wa Ofisi ya Wizara ya Viwanda na Biashara katika mji wa Serikali wa Mtumba mkoani Dodoma, kushoto ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Hassan Mohamed.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akiongozwa na Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Grace Musita kukagua ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika mji wa Serikali eneo la Mtumba Dodoma .


 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula katikati akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa ofisi ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika mji wa Serikali wa Mtumba kutoka kwa Mkurugenzi wa uendelezaji milikShirika la Nyumba la Taifa Haikameni Mlekio wakati alipofanya ziara, kushoto ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Grace Musita.