ON POINT MEDIA

ON POINT MEDIA
Karibuni sana kwa kazi nzuri ya video za harusi mikutano na kadharika

SHIRKA LA NYUMBA LA TAIFA

SHIRKA LA NYUMBA LA TAIFA
NYUMBA YANGU MAISHA YANGU

Monday, 3 December 2018

MKURUGENZI MKUU NHC AFANYA ZIARA KATIKA MKOA WA MOROGORO

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Dkt. Maulidi Banyani alifanya ziara ya siku mbili katika mkoa wa Morogoro na kutembelea miradi mbalimbali akianzia katika Halmashauri ya wilaya ya Malinyi ambapo Shirika la nyumba la Taifa linajenga jengo la Halmashauri  ya wilaya ya Malinyi kama Mkandarasi,
Mkurugenzi Mkuu Dkt. Maulidi Banyani ameagiza ifikapo  tarehe 29/05/2019 jengo liwe limekamilika na kukabidhiwa kwa Halmashauri.

Baada ya kutoka katika Halmashauri ya wilaya ya Malinyi ziara hiyo ilielekea katika wilaya ya Mvomero ambapo shirika limejenga nyumba  42. 

Vilevile Mkurugenzi Mkuu Dkt. Banyani alitembelea Jengo la biashara na ofisi la 2D lililopo Morogoro Mjini, Dkt. Banyani alitoa agizo kwa Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa, Verenanda Seif kuhakikisha wanalitangaza jengo hilo ili lipate wapangaji wa kutosha tofauti na sasa ambapo asilimia 30 tu ndio iliyochukuliwa sehemu kubwa ikiwa ni mabenki
pia akatoa agizo kwa mameneja wote pindi wanapopangisha jengo wawe wanapiga picha jengo kabla ya mpangaji kuingia ili anapoondoka akabidhi likiwa bora kama alivyokabidhiwa na si vinginevyo.
Pia alitembelea Plot No 31- 34 Nkomo, Plot No 66/2 OLD DSM ROAD, PLOT 53 KINGO  mwisho alimaza ziara kwa kutembelea Shule ya Sekondari Mzumbe iliyokarabatiwa na Shirika. Mkuu wa Shule alilipongeza Shirika kwa kufanya kazi nzuri na yenye weledi na kutoa wito kwa Serikali kwa miradi kama hiyo wapewe NHC kwani wamefanyakazi nzuri sana na kwa wakati.

Jengo la Halmashauri  ya wilaya ya Malinyi linavyoonekana kwa sasa
Dkt. Maulidi Banyani akiwa ameongozana na Kaimu Mkuu wa kitengo cha ukaguzi wa ndani Abdallah Migila pamoja Meneja wa mkoa wa Morogoro Veneranda Seif wakiwa katika mradi wa jengo la Halmashauri  ya wilaya ya Malinyi.


Mhandisi Hassan Mohamed akitoa maelezo ya mradi kwa Mkurungezi Mkuu NHC Dkt. Maulidi Banyani 



Mhandisi Hassan Mohamed akitoa maelezo ya mradi kwa Mkurungezi Mkuu NHC Dkt. Maulidi Banyani



Mkurungezi Mkuu NHC Dkt. Maulidi Banyani akitoa maelekezo wakati alipotembelea mradi huo wa jengo la Halmashauri  ya wilaya ya Malinyi unaotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa.
Mkurugenzi Mkuu Dkt. Maulidi Banyani akimkaribisha Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri  ya wilaya ya Malinyi Mussa Mnyeti  alipotembelea katika mradi wa jengo Halmashauri  ya wilaya ya Malinyi linalojengwa na NHC 


Picha ya pamoja kati ya watumishi wa  Halmashauri  ya wilaya ya Malinyi na Shirika la Nyumba la Taifa.


Mkurugenzi Mkuu Dkt. Maulidi Banyani akiwa  na Kaimu Mkuu wa kitengo cha ukaguzi wa ndani Abdallah Migila, Baraka Killungu  wakiwa na  Meneja wa mkoa wa Morogoro Veneranda Seif wakiwa katika  Nyumba za makazi Mvomero.

Nyumba za makazi 42 zilizojengwa  katika Halmashauri ya wilaya ya Mvomero
Mkurugenzi Mkuu NHC Dkt. Maulidi Banyani wakijadiliana jambo  na Kaimu Mkuu wa kitengo cha ukaguzi wa ndani Abdallah Migila walipotembelea Nyumba za makazi 42 zilizojengwa  katika Halmashauri ya wilaya ya Mvomero

Muonekano wa Jengo la biashara na ofisi la 2D Morogoro 

Mkurugenzi Mkuu NHC Dkt. Maulidi Banyani akitoa maelezo alipotembela jengo la biashara na ofisi la 2D Morogoro .



    PLOT NO. 31-34 NKOMO, eneo lenye  Magodown  mawili  ambayo hayatumiki kwa sasa kutokana na kuchakaa kwa magodown hayo.

Mkurugenzi Mkuu NHC Dkt. Maulidi Banyani akiwa ndani ya jengo la godown

PLOT NO 66/2 OLD DSM ROAD

PLOT NO 66/2 OLD DSM ROAD


PLOT NO 53KINGO

Mkuu wa shule ya Sekondari Mzumbe akimkaribisha Dkt. Maulidi Banyani Mkurugenzi Mkuu NHC alipotembelea shuleni hapo.

Moja ya jengo lilikarabatiwa na Shirika la Nyumba la Taifa 



No comments:

Post a Comment