ON POINT MEDIA

ON POINT MEDIA
Karibuni sana kwa kazi nzuri ya video za harusi mikutano na kadharika

SHIRKA LA NYUMBA LA TAIFA

SHIRKA LA NYUMBA LA TAIFA
NYUMBA YANGU MAISHA YANGU

Friday, 22 July 2016

SHIRIKA LA NYUMBA LAIKABIDHI BENKI KUU MAJENGO KWA AJILI YA WAFANYAKAZI WAKE MTWARA

Benki Kuu ya Tanzania imekabidhiwa jengo la ghorofa tano lililojengwa na NHC eneo la Shangani Mtwara,  lenye nyumba kumi ilizonunua kwa ajili ya Wafanyakazi wake wanaotarajiwa kuhamia Mtwara mwezi Septemba mwaka huu ikiwa ni ishara ya Benki hiyo kuanza kutoa huduma katika kanda ya kusini mwa Tanzania. Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prefesa Benno Ndulu amelishukuru Shirika la Nyumba kwa kuwajengea nyumba bora za kisasa. Aidha, Benki Kuu ya Tanzania imenunua nyumba 40 zinazojengwa na NHC eneo la Rahaleo Mtwara ambazo zinatarajiwa kukabidhiwa mwezi Septemba mwaka huu.


 Jengo la ghorofa tano ambalo NHC imeikabidhi Benki kuu ya Tanzania eneo la Shangani Manispaa ya Mtwara.

 Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akimkaribisha Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prefesa Benno Ndulu alipowasili eneo la shangani kukabidhiwa Nyumba walizonunua.


 Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu aliongea na hadhira wakati wa sherehe ya kuikabidhi Benki Kuu ya Tanzania Nyumba walizonunua kwa ajili ya wafanyakazi wa banki hiyo.


                               Viongozi wandamizi kutoka Banki kuu ya Tanzania

 Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prefesa Benno Ndulu akitoa neno la shukrani kwa uongozi wa  Shirika la Nyumba kwa kuwajengea nyumba bora za kisasa.

Gavana wa Benki Kuu na Mkurugenzi Mkuu wa NHC wakisaini hati ya kukabidhiana nyumba zilizonunuliwa na Banki Kuu eneo la Shangani Mtwara.

 Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akimkabidhi Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prefesa Benno Ndulu Cheti cha ubora wa Jengo kuashiria kuwa jengo lao walilonunua NHC ni salama kukaliwa na wafanyakazi wa Banki hiyo.
  Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akimkabidhi Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prefesa Benno Ndulu mfano wa  ufunguo wakati alipo mkabidhi nyumba walizo nunua kwa ajili ya watumishi wa Banki Kuu tawi la Mtwara.

 Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prefesa Benno Ndulu akikata utepe kuashilia kukabidhiwa Nyumba walizonunua kwa ajili ya wafanyakazi wa Banki Kuu tawi la Mtwara.


Picha ya pamoja ya Viongozi wa NHC na BOT baada ya  kukabidhiana nyumba za makazi zilizojengwa na NHC eneo la Shanghai Mtwara

 Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akimuonyesha Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prefesa Benno Ndulu Mazingira ya nyumba hizo.




 Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Ndg. Julian Banzi Raphael na Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu wakifurahia jambo walipotembelea mradi wa Rahaleo Mtwara, Ambapo Benki Kuu ya Tanzania imenunua nyumba za makazi 40 kwa ajili ya  watumishi wa Banki Kuu tawi la Mtwara.


 Mkrugenzi wa Ujenzi Mhandisi Haikamen Mlekio akimuhakikishaia Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prefesa Benno Ndulu kuwa nyumba 40 zilizobaki zitakamilika kwa wakati waliokubaliana

No comments:

Post a Comment